Saturday 27 August 2011

Mapishi ya Maini ya kuku



Mahitaji
Maini ya kuku 1/2 kilo
Vitunguu vikubwa 2
Hoho 1
Pilipil 1
Limao 1/2
Swaum/tangawizi 1 kijiko cha chai
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Mafuta ya kupikia

Matayarisho
Safisha maini weka pembeni. Baada ya hapo kaanga vitunguu,swaum na tangawizi pamoja (hakikisha vitunguu visiwe vya brown), kisha tia maini, curry powder, pilipili, chumvi ,hoho na limao kisha changanya vizuri na ufunike. Pika mpaka maini yaive na hakikisha yanakuwa na rojo kidogo. Baada ya hapo ipua na yatakuwa tayari kwa kuliwa na chochote upendacho kama vile chapati, chips, ugali, wali.

3 comments:

  1. iko vizur mama ntilie

    ReplyDelete
  2. nnpenda sana limao/ndimu karibia kila chakula napikia,kama wewe

    ReplyDelete
  3. nnpenda sana limao/ndimu karibia kila chakula napikia,kama wewe

    ReplyDelete