Thursday 19 May 2011

Jinsi ya kupika Sambusa za vegetable


Mahitaji
Viazi 6 vya wastani
Hoho jekundu 1/2
Hoho la kijani 1/2
Vitunguu maji 2 vikubwa
Njegere 1/2 kikombe
Carrots 2 zilizo kwanguliwa
Garlic/ ginger paste 1 kijiko cha chai
Curry powder 1/2 kijiko cha chai
Corinder powder 1/4 kijiko cha chai
Turmaric 1/4 kijiko cha chai
Chilli powder kiasi
Limao 1/2
Chopped coriander kiasi
Chumvi
Manda
Mafuta ya kukaangia

Matayarisho
Menya viazi kisha vichemshe na chumvi kidogo. Vikiiva vimash na uma mpaka vilainike kiasi kisha viweke pembeni. Baada ya hapo katika sufuria isiyoshika tia mafuta kidogo sana. Yakipata moto tia vitunguu maji kaanga kwa muda wa dk 2 kisha ginger/garlic paste kaanga kidogo kisha tia spice zote. Zichanganye vizuri. Baada ya hapo tia vegetable zote zilizobaki pamoja na chumvi, limao zipike pamoja kwa muda wa dk 5.Malizia kwa kutia mashed potato na vimaji kidogo sana. Zichanganye vizuri mpaka vitu vyote vichanganyike kisha ipua. Acha vipoe kisha tia coriander.Baada ya hapo funga kama unavyokunja sambusa za kawaida kisha zichome ktk mafuta.Zikisha iva zitakuwa tayari kwa kuliwa.

Note:
Inapendeza zaidi vegetable zote (kasoro carrot) kukatwa ktk shape ya cubes ndogondogo.

No comments:

Post a Comment