Wednesday 18 August 2010

Mapishi ya Supu ya samaki,viazi na broccoli

Mahitaji

  • Samaki mbichi 1
  • Viazi mbatata (potato 2)
  • Broccoli (kiasi)
  • Nyanya (Fresh tomato 1)
  • Kitunguu (onion 1/2)
  • Chumvi (salt 1/4 kijiko cha chai)
  • Limao (lemon 1/4)
  • Pilipili (chilli 1 nzima)
  • Mafuta (vegetable oil)
Matayarisho
Safisha samaki na umkate vipande 3. Menya viazi na kisha vikate vipande vya wastani, Pia katakata nyanya, kitunguu na broccoli kisha weka pembeni. Chukua sufuria kisha tia viazi na maji kiasi kisha vichemche kiasi karibia kuiva. Baada ya hapo tia samaki, kitunguu, nyanya, broccoli, chumvi limao,pilipili na mafuta kidogo. Acha supu ichemke mpaka viazi na samaki viive kisha supu itakuwa tayari.

No comments:

Post a Comment