Wednesday 27 April 2011

Jinsi ya kupika Fish cakes


Mahitaji
Fish fillet (steki ya samaki isiyokuwa na mifupa) kipande 1 kikubwa
Viazi (potato) 6 vya wastani
Kitunguu (onion) 1 kikubwa
Tangawizi na swaum (garlic and ginger paste) 1 kijiko cha cha chai
Breadcrumbs kiasi
Mayai (eggs) 2
Limao (lemon) 1/2
Chumvi (salt) kiasi
Pilipili (scotch bonnet chilli) 1/4
Curry powder 1/2 cha chai
Coriander powder 1/4 kijiko cha chai
Turmaric 1/4 kijiko cha chai
Fresh chopped coriander kiasi.
Mafuta ya kukaangia

 Matayarisho
Chemsha viazi na chumvi kidogo kisha viponde na uviweke pembeni vipoe.Katakata samaki vipande kisha mtie kwenye sufuria pamoja na tangawizi, swaum, limao na chumvi. Mchemshe kidogo(hakikisha maji yote yanakauka) kisha mponde na uma (folk) baada ya hapo tia spice zote,pilipili na vitunguu vilivyokatwa vidogovidogo na uvipike pamoja na samaki kwa muda wa dk 3. Baada ya hapo tia coriander na kamulia limao kisha viweke pembeni. Baada ya hapo changanya viazi pamoja na mchanganyiko wa samaki kisha tengeneza maduara ya wastani. Baada ya hapo piga mayai ktk bakuli na chumvi kidogo.Bandika jikoni mafuta  ya kukaangia ktk fry pan yawe kidogo tu (shallow fry) yakisha pata moto kiasi chukua madonge yako kisha yachovye ktk mayai na umalizie ktk breadcrumbs kisha zikaange ktk mafuta. Baada ya hapo zitakuwa tayari kwa kuliwa

No comments:

Post a Comment