Monday 14 March 2011

Mapishi ya Kofta curry


Mahitaji
Vitu vya kofta
Nyama ya kusaga (minced beef) 1/4 kilo
Yai (egg) 1
Kitunguu maji (chopped onion) 1
Kitunguu swaum/ tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko cha chakula
Garam masala powder 1 kijiko cha chai
Pilipili ya unga (chilli powder) 1/2 ya kijiko cha chai
Limao (lemon) 1/2
Breadcrumbs 3 vijiko vya chakula
Chumvi (salt)

Vitu vya curry
Tui la nazi (coconut milk) kopo 1
Nyanya (fresh tomato) 2
Kitunguu (onion) 1
Kitunguu swaum/tangawizi (ginger and garlic paste) 1 kijiko cha chai
Curry powder 1 kijiko cha chai
Coriander powder 1/2 kijiko cha chai
Turmaric 1/2 ya kijiko cha chai
Chumvi (salt)
Mafuta (veg oil) kiasi
Giligilani (coriander)

Matayarisho
Changanya nyama na vitu vyake vyote kisha iache kwa muda wa 1/2 saa ili iingie viungo. Baada ya hapo tengeneza maduara na uyapange kwenye baking tray kisha zichome kwenye oven mpaka ziive. Baada ya hapo saga pamoja nyanya, kitunguu, swaum na tangawizi. kisha vitie kwenye sufuria na upike mpaka maji yote yakauke, kisha weka mafuta kidogo, chumvi na spices zote koroga mpaka vichanganyike vizuri kisha tia tui la nazi. Liache lichemke mpaka libakie kidogo na umalizie kwa kutia kofta. Zichanganye vizuri na huo mchuzi kisha ziache zichemke kidogo na uipue. Malizia kwa ku garnish na coriander na hapo kofta curry yako itakuwa tayari kwa kuliwa. Unaweza kula kwa wali, ugali, viazi au chapati.




1 comment:

  1. Hii ni kama meatballs? Kwa kweli napenda sana mapishi yako (recipes), very simple, delicious and easy to cook. Tuko pamoja!

    ReplyDelete