Saturday 14 August 2010

Mapishi ya Uji wa ulezi



Mahitaji

  • Unga wa ulezi (millet flour vijiko 3 vya chakula)
  • Maziwa fresh (milk 1/2 kikombe)
  • Sukari (sugar 1/4 ya kikombe cha chai)
  • Siagi (butter kijiko 1 cha chakula)
  • Maji (vikombe 4 vya chai) (serving ya watu wawili)
Matayarisho
Chemsha maji ya uji, Kisha koroga unga na maji ya baridi kiasi na uchanganye kwenye maji ya moto yanayochemka. Endelea kukoroga mpaka uchemke ili kuhakikisha uji haupatwi na madonge. Ukishachemka tia, maziwa, sukari na butter. Kisha acha uchemke kwa muda wa dakika 10 na hapo uji utakuwa tayari.

1 comment: