Tuesday 3 August 2010

Mchemsho wa samaki na viazi



Mahitaji


  • Samaki mbichi (1)
  • Viazi mbatata (3)
  • Nyanya (1)
  • Kitunguu maji
  • Limao
  • Kitunguu saumu 
  • Tangawizi
  • Chumvi
  • Pilipili
  • Vegetable oil
Matayarisho

Safisha samaki kisha mmarinate na tangawizi, kitunguu swaum, chumvi na limao kwa muda wa masaa mawili. Baada ya hapo menya viazi na uvikate vipande vidogo kisha vioshe na viweke kwenye sufuria yenye maji kiasi kwa ajili ya kuvichemsha. Viinjike jikoni na uviache vichemke kwa dakika 7. Vikisha chemka tia samaki, katia kitunguu,pilipili, chumvi, limao, vegetable oil na nyanya na uache supu ichemke mpaka samaki na viazi vitakapoiva. baada ya hapo supu itakuwa tayari kwa kuliwa.

No comments:

Post a Comment